Feb 17, 2012

YUSUF RAZA GILANI: Apandishwa kizimbani kwa kukataa kuchunguza ufisadi wa mkuu wake

Yousaf Raza Gillani

Pakistan

MAHAKAMA kuu nchini Pakistan imetupilia mbali rufaa ya waziri mkuu wa nchi hiyo dhidi ya mashitaka yanayomkabili ya kudharau mahakama. Ina maana kuwa Yusuf Raza Gilani (pia huandikwa Yousaf Raza Gillani) atatakiwa kufika mbele ya mahakama kuu kusikiliza mashitaka dhidi yake ya kukataa kuchunguza tuhuma za ufisadi zinazomkabili rais wa nchi hiyo.

Waziri Mkuu hakuwa mahakamani siku kesi yake ilipotajwa, lakini wakili wake alisema Yusuf Raza Gilani hakudharau mahakama kwa kukataa kuchunguza madai ya ufisadi dhidi ya rais. Wakili huyo wa waziri mkuu, alisema Rais Asif Ali Zardari, akiwa mkuu wa nchi, sheria zinamlinda kutoshitakiwa.

Historia yake

Yusuf Raza Gilani (Mbunge) alizaliwa Juni 9, 1952, ni Waziri Mkuu wa 16 na wa sasa wa Pakistan, na makamu mwenyekiti wa chama cha kijamaa cha kidemokrasia, Pakistan Peoples Party (PPP). Gilani alipendekezwa kuhudumu katika ofisi ya ofisi ya waziri mkuu na kuwa waziri mkuu wakati chama chake kilipoanzisha serikali ya umoja na Pakistan Muslim League, Awami National Party, Assembly of Islamic Clergy na Muttahida Qaumi Movement (MQM), baada ya chama chake kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa Bunge wa 2008. Ni waziri mkuu wa kwanza kutoka ukanda wa Wapakistanbi wanaozungumza lugha ya Saraiki, na pia waziri mkuu aliyehudumu kwa kipindi kirefu cha miezi 45 na kuongoza zaidi ya vikao 100 vya Bunge na baraza la mawaziri; mafanikio makubwa zaidi ya serikali ya kidemokrasia katika historia ya nchi hiyo.

Mafanikio yake ya kwanza yalikuwa kugombea ubunge 1988 na amekuwa mbunge mwandamizi wa jimbo la Multan-IV tangu mwaka 1988, akiongoza Wizara ya Utalii chini ya serikali ya waziri mkuu wa zamani, Benazir Bhutto. Baada ya chama chake kushinda katika uchaguzi wa bunge wa 1990, Gilani aliteuliwa na Benazir Bhutto kuwa Spika wa 15 wa Bunge, alihudumia hadi Februari 16, 1997. Februari 11, 2001, Gillani alifungwa na mahakama ya kijeshi akiweka chini ya Rais Pervez Musharraf, kwa shutuma na tuhuma za rushwa katika jela isiyofahamika sana ya Adiala, na alitolewa Oktoba 7, 2006.

Chama cha Gilani, PPP, kilipata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa bunge wa mwaka 2008, na kwa ridhaa ya serikali ya mseto, Gilani aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu, akila kiapo kutoka kwa Rais Pervez Musharraf, tarehe 25 Machi, 2008. Katika kikao cha kwanza cha uzinduzi, Gilani alitangaza kuundwa kwa tume ya Ukweli na upatanisho, kupunguza bajeti na matumizi ya serikali, ujenzi wa ukanda ulioharibiwa kwa ukabila, elimu, ardhi, na mageuzi ya kilimo, ikifuatiwa na sera mpya ya nishati ya nyuklia. Mwaka 2009, Gilani aliwekwa katika nafasi ya 38 kama mtu mwenye mamlaka zaidi duniani na jarida la Forbes.

Asili yake

Gillani ni wa asili ya Iran na baba yake alikuwa mzao wa Syed Musa Pak, mtu wa imani ya kiroho ya Qadiri Sufism ambayo ilifuata asili yake kwa Abdul-Qadir Gilani wa Iran. Babu wa Yousaf Raza wa upande wa baba anatoka jimbo la Paktia, Afghanistan, lakini akaweka makazi nchini Iran baada ya kumuoa mwanamke wa Iran. Familia yake ilihamia Multan mwaka 1921 na baba yake Alamdar Hussain Gilani alikuwa kiongozi wa kisiasa wa Multan ambaye alitoa mchango mkubwa katika siasa za Pakistan. Hussain Gilani alikuwa mmoja wa watia saini wa Azimio la Pakistan mwaka 1940, na aliwahi kuongoza harakati za Pakistan. Mwaka 1953, Alamdar Hussain Gilani alikuwa waziri wa muda kwa Feroz Noon Khan, na pia alikuwa Waziri wa baraza la mawaziri baada ya Feroz Khan Noon kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu mwaka 1958.

Elimu na familia

Gilani alizaliwa Juni 9, 1952 mjini Karachi, jimbo la Sindh, Magharibi mwa Pakistan. Muda mfupi tu, Gilani alihamia Multan, Jimbo la Punjab, alihudhuria mafunzo katika Chuo Kikuu cha Kikristo cha Forman. Alihudhuria katika Chuo cha Serikali na kupata shahada ya kwanza (BA) katika Uandishi wa Habari, na kufuatiwa na shahada ya uzamili (MA) katika Uandishi wa Habari wa Siasa kutoka Chuo Kikuu cha Punjab.

Gilani ameoa na ana watoto watano, wanne wa kiume, binti mmoja, na mmoja mjukuu. Mtoto wake mkubwa, Syed Abdul Qadir Makhdoom Gilani, alianzia kazi yake ya siasa Multan, na mwaka 2008, alimuoa mjukuu ya Pir Pagara Shah Mardan Shah II, kiongozi wa kisiasa na kidini wa Sindh mwenye ushawishi mkubwa. Watoto wake wengine watatu wa kiume, Ali Qasim Gilani, Ali Musa Gilani na Ali Haider Gilani walizaliwa mapacha watatu. Qasim Gilani kwa sasa anachukua shahada ya kwanza kutoka Chuo Kikuu cha Brunel London, ambapo Musa Gillani amemaliza shahada yake ya pili kutoka Chuo Kikuu Queen Mary cha London mwaka 2009.  Ali Haider Gilani anasoma katika Shule ya Uchumi ya Lahore, iliyopo Lahore.  Ali Musa Gilani baada ya kumaliza masomo yake kwa sasa anashiriki kikamilifu katika siasa. Jina la binti wa Yousaf Raza Gilani, ni Fiza Gillani.

Umma mtumishi

Kazi ya siasa ya Gilani ilikatishwa wakati wa sheria ya kijeshi wa Jenerali Zia-ul-Haq mwaka 1978, wa kwanza kujiunga na Kamati Kuu ya Pakistan Muslim League (PML), pamoja na Nawaz Sharif. Lakini hivi karibuni alijiondoa PLM, kutokana na tofauti za kisiasa.

Alichaguliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Taifa (MNA) kwa mara ya kwanza akitokea Lodhran, kiti kinachoshikiliwa kwa sasa Saddique Baloch NA 154. Alikuwa pia mwanachama wa baraza la mawaziri katika serikali ya miaka mitatu ya Gilani akijiunga na Pakistan Peoples Party (PPP) mwaka 1988, kutokana na tofauti na Nawaz Sharif. Benazir Bhutto alichangia kwa kiasi kikubwa katika falsafa ya kisiasa ya Gilani na alikuwa waziri katika serikali ya Benazir Bhutto ya 1988-1990, alichaguliwa tena katika Bunge la Taifa kutoka kiti kingine NA 152, ambacho kwa sasa kinashikiliwa na Nawab liaqat ali, na alikuwa Waziri wa Utalii kutoka Machi 1989 hadi Januari 1990 na Waziri wa Nyumba na Ujenzi kuanzia Januari 1990 hadi Agosti 1990.  Baadaye, chini ya serikali nyingine ya Bhutto, akawa Spika wa Bunge mwezi Oktoba.

Kifungo

Yousaf Raza Gilani alikamatwa tarehe 11 Februari 2001, chini ya Ofisi ya Taifa ya Uwajibikaji (NAB), taasisi ya kupambana na rushwa, iliyoanzishwa na serikali ya kijeshi mwaka 1999, kwa madai kwamba alitumia vibaya mamlaka yake alipokuwa Spika wa wa Bunge. Hasa, alidaiwa kukodisha hadi watu 600 kutoka miongoni mwa wananchi wa jimbo lake na kuwaweka katika orodha ya mishahara ya serikali. NAB ilidai kuwa Gilani alisababisha hasara ya Rupia milioni 30 kila mwaka katika hazina ya taifa. Alikutwa na hatia na mahakama ya kupambana na rushwa iliyoundwa na Musharraf na alitumikia kifungo cha karibu miaka sita gerezani.

Jaribio la mauaji 2008

Gilani alikoswa kuuawa baada ya jaribio la mauaji lililofanywa tarehe 3 Septemba 2008, wakati mtu mwenye silaha asiyejulikana aliposhambulia gari lake lisilopenya risasi karibu na jiji la Rawalpindi, taarifa rasmi zimebainisha. Jaribio hilo lilitokea muda mfupi baada ya Gillani kurudi akitokea katika ziara ya kiofisi katika jiji la mashariki la Lahore. Msafara wake ulikuwa ukielekea Islamabad kutokea eneo la jeshi lenye ulinzi mkali la Rawalpindi. Msemaji wa Waziri Mkuu alisema Gilani na wafanyakazi wake hawakujeruhiwa.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa.

No comments:

Post a Comment