Nov 30, 2011

ETIENNE TSHISEKEDI: Mwanasiasa mwenye matatizo ya kiafya wa DRC asiyechuja

 Etienne Tshisekedi wa Mulumba

KINSHASA
Congo

UPIGAJI kura katika uchaguzi mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), ulifanyika mapema wiki hii. Uchaguzi huo wa rais na wabunge ni wa pili kufanyika nchini humo baada ya kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka minane iliyopita.

Hata hivyo muda wa upigaji kura uliongezwa na kuingia siku ya pili katika baadhi ya maeneo sehemu ambazo upigaji huo haukufanyika siku ya Jumatatu. Maafisa wa uchaguzi walisema kuongeza muda huo kuliathiri takriban watu 400 katika nchi hiyo kubwa yenye vituo vya kupigia kura 63,000.

Mbali na hatua hiyo kuchukua muda mrefu, upigaji kura huo uligubikwa na vurugu huku vituo vya kupigia kura vikishambuliwa na watu wenye silaha na wapiga kura wenye hasira. Ni uchaguzi wa pili tangu kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka minane iliyopita, ambapo watu milioni nne walifariki dunia.

Wote wawili rais Joseph Kabila, mwenye umri wa miaka, 40, ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 10, na kiongozi wa upinzani mkongwe, Etienne Tshisekedi, mwenye miaka, 78, wamesema wanaamini watashinda. Tshisekedi amemshutumu Bw Kabila kwa kupanga kuutia hila uchaguzi.

Historia ya Tshiseked

Etienne Tshisekedi wa Mulumba amezaliwa 14 Desemba 1932, ni mwanasheria, mwanasiasa, na kiongozi wa chama cha UDPS. Alikuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo (wakati ikiitwa Zaire) mara tatu: 1991, 1992-1993, na 1997.

Tshisekedi alizaliwa pale Luluabourg (sasa inaitwa Kananga), Kasai mwaka 1932, akiwa ni mwana wa Alexis Mulumba na mke wake Agnès Kabena. Anatokea katika kabila la Luba. Alihitimu stashahada (diploma) mwaka 1961 katika Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Lovanium cha Léopoldville (sasa Kinshasa). Aliwahi kufanya kazia katika serikali ya Mobutu katika nafasi mbalimbali kwenye miaka ya 1960 na 1970.
Kwa sasa ndiye mpinzani mkuu wa Rais Kabila katika Uchaguzi wa wa Rais nchini Kongo. Tshisekedi alitoa taarifa mnamo Novemba 2011 akijitangaza kuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kazi ya siasa
Mwaka 1960, Tshisekedi, aliyekuwa kamishina msaidizi katika Chuo cha Mobutu cha Makamishna, alishiriki katika mazungumzo kati ya Léopoldsville, Élisabethville na Bakwanga kuhusu makabidhiano ya Patrice Lumumba (ambaye alikuwa chini ya ulinzi wa Mobutu) aidha kwa Moise Tshombe au Albert Kalonji ili kumuondoa Lumumba.

Muda mfupi kabla ya Krismasi, Tshisekedi alimtumia taarifa ya kidiplomasia Albert Kalonji ambapo alijadili makabidhiano ya wafungwa wengine wa kisiasa na jinsi watakavyopokea adhabu ya kifo. Mapema Mukamba, kamishina wa Kalonji, alielezea kwa undani kile ambacho kingemtokea Lumumba kama Albert Kalonji atajiingiza kwenye uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia wa uwaziri mkuu wa Kongo mkuu: "Lumumba Patrice atahamishiwa Bakwanga na kwenye mji huo angeuawa na kukatwa katika vipande vidogo ambavyo kila m-Luba angekuwa na uwezo wa kula nyama yake."
Taarifa ifuatayo, ilivuja kutoka kwa Mobutu kwenye magazeti ya Kongo katika miaka ya 1990, na ilitumwa na Tshisekedi mnamo Desemba 1960 na ilisomeka kama ifuatavyo:
BARAZA LA MAWAZIRI LA WIZARA YA SHERIA
N°1.399/ETSH/ ME/CAB.
Mtukufu Mfalme wa Kasai Kusini "Mulopwe"
Kwa Bakwanga
Nawasilisha heshima yangu kwako Mtukufu kwamba sasa yule chura (akimaanisha Patrice Lumumba aliyewekwa jela na Mobutu) amezingatiwa, jitihada ya Timu yetu bado inatafakari katika imani yote kuhusu washirika wake wa zamani ili kuzuia uendelevu wa kazi yake ya uharibifu. Hivi karibuni, serikali yako mtukufu wa enzi itamilki maluteni muhimu wa chura ambao ni Pierre Elengesa, Jean-Pierre Finant, Emmanuel Nzuzi, Christophe Muzungu, Joseph Mbuyi ili kuwafanya wakabiliane na adhabu itakayokuwa ya mfano. Ni katika njia hii ya kufanya kazi tutasaidia vita unavyopigana. Kwa heshima yangu yote Mtukufu…

Naibu Kamishna wa Haki
E. TSHISEKEDI E. TSHISEKEDI
Mnamo Februari 9, 1961, wafungwa 6 wa kisiasa ambao Tshisekedi aliwamaanisha walisafirishwa kwenda Bakwanga, eneo lililo chini ya udhibiti wa Albert Kalonji kukutana na kile kilichoelezwa kabla na Mukamba. Wafungwa hao 6 wa kisiasa walikuwa: Jean-Pierre Finant, Jacques Fataki, Pierre Elengesa, Camille Yangara, Emmanuel Nzuzi na Christophe Muzungu.”
Mwaka 1980 Tshisekedi aliondolewa kwenye serikali ya Mobutu na kutupwa gerezani kwa ukosoaji. Baada ya hapo akaendelea kutupwa ndani mara kwa mara na serikali zote mbili, ya Mobutu na Laurent Kabila. Mwaka 1989 wakati bado serikali ikiwa chini ya Mobutu, kesi kadhaa za kuzuiliwa kwake zilitambuliwa kuwa ni kinyume cha sheria na Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa.

Tarehe 15 Februari 1982 alianzisha chama cha UDPS, ambacho bado anaendelea kukiongoza. Chama kimeendelea kuwa maarufu miongoni mwa watu wa kabila la Tshisekedi la wa Kasai na lengo lake kuu ni kuwa na mabadiliko yasiyokuwa na ghasia kuelekea utawala wa kidemokrasia. Kwa mujibu wa Thomas Luhaka wa MLC, nguvu kubwa ya UDPS na viongozi wake ni uhusiano wa karibu na watu wenye ushawishi mkubwa katika vyombo vya habari nchini humo ikiwa ni pamoja na “Le Potentiel,” “Le Phare,” na “La Tempete des Tropiques”.

Hili lilithibitishwa na balozi wa Marekani nchini Kongo, Roger Meece, ambaye alidai "Le Phare" na "La Temptete" kimsingi yanahusiana na UDPS. [12] Katika mtandao, balozi Meece pia aliandika kwamba ingawa wanachama UDPS hupenda kutaja "demokrasia", "maadili ya jamhuri" na "utawala wa sheria", UDPS kama chama cha siasa kipo mbali na demokrasia na kwamba msimamo wake ni kupambana na hata kukiuka mikataba ya kisiasa.

Tshisekedi aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu mara tatu tofauti. Mara ya kwanza alidumu kwa mwezi mmoja tu (Septemba 29, 1991 - 1 Novemba 1991), ya pili kwa muda wa miezi saba (15 Agosti 1992 - 18 Machi 1993). Mara zote, Tshisekedi alilalamika kwamba alizuiwa kufanya kazi vizuri na Mobutu. Awamu ya tatu, ilikuwa wakati vikosi vya waasi vya Laurent Kabila vilipokuwa vikiandamana Kinshasa, alidumu kwa wiki tu (2 Aprili 1997 - Aprili 9, 1997) na alikosa tena ushirikiano kutoka kwa Mobutu. Mwezi mmoja baadaye Laurent Kabila alimuondoa madarakani Mobutu.

Uchaguzi wa 2011

Katika mkutano wa UPDS mwezi Aprili, 2009, wajumbe bila kupingwa waliamua kuwa chama kitashiriki katika uchaguzi wa 2011 na Tshisekedi atakuwa mgombea wake wa urais. Agosti 2011, Tshisekedi alitangaza kutaka majadiliano na vyama vingine vya upinzani ili kuunda juhudi za pamoja dhidi ya rais anayemaliza muda wake, Joseph Kabila. Hii ni mara ya kwanza ya Tshisekedi kugombea urais wa nchi hiyo tangu kuanzisha chama cha upinzani cha kwanza mwaka 1982.

Tshisekedi anayekaribia miaka themanini afya yake ni mbaya. Katika muongo uliopita alifanyiwa mfululizo matibabu ya nchini Afrika Kusini na Ubelgiji. Akitokea Afrika Kusini, Tshisekedi ana matatizo ya kutembea kwa sababu uwezo wake wa kuona umeshuka kwa kiasi kikubwa. Masamba pia alisema kwamba uwezo wa akili wa Tshisekedi umepungua. Kwa sababu ya afya yake mbaya, pia mara chache amekuwa akionekana kwa umma. Mukamba alisema kuwa Tshisekedi “hatamaliza miaka miwili” katika harakati. Waangalizi wengi wa kujitegemea wanakubaliana kwamba Tshisekedi akifa, UDPS itaanguka, lakini kwa yu hai wanachama wa UDPS watajaribu kumtumia kwa vyovyote iwezekanavyo.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa

No comments:

Post a Comment