Jan 4, 2012

YOUSSOU N'DOUR: Msanii na mwanaharakati anayeutaka urais wa Senegal

Youssou N'dour

DAKAR
Senegal

MWANAMUZIKI mashuhuri nchini Senegal na mwanaharakati wa kisiasa, Youssou N'dour, ametangaza kuwa atawania kiti cha urais katika uchaguzi wa mwezi Februari nchini humo.

Mwanamuziki huyo amesema kuwa anaitikia wito wa kumtaka agombee kiti hicho dhidi ya rais wa sasa Abdoulaye Wade, ambaye anapania kuwania kiti hicho kwa muhula wa tatu.

Youssou N'dour amekuwa akijihusisha na masuala ya kibinadamu kwa siku nyingi na pia ni balozi wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu masuala ya watoto (UNICEF).

Mwandishi wa BBC mjini Dakar, Thomas Fessy, amesema kuwa hatua ya Youssou N'dour kutangaza kuwa atawania kiti cha urais, haijawashangaza wengi. Hii ni kufuatia tangazo alilotoa mwisho wa mwaka uliopita kuwa atajitosa katika ulingo wa kisiasa.

Katika hotuba iliyorushwa kupitia kituo chake cha redio na televisheni, mwanamuziki huyo ambaye pia ni mfanyabiashata mwenye mafanikio amesema atapunguza matumizi ya serikali na kuahidi kuzalisha chakula na umeme kwa wote iwapo atachaguliwa kuwa rais wa Senegal.

Youssou N'dour anakubali kuwa yeye sio msomi lakini anaelezea wadhifa wa urais kuwa ni ''kazi na sio taaluma''.

Youssou N'dour alikuwa rafiki wa karibu wa Rais Abdoulaye Wade, lakini baada ya Wade kutangaza nia ya kuwania kiti cha urais kwa muhula wa tatu, aligeuka na kuwa mpinzani wake mkuu.

Na amekuwa akisema kwamba Wade anatakiwa kutogombea mhula mwingine wa tatu kwa sababu anavunja katiba.

Lakini haitakuwa kazi rahisi kwa Youssou Ndour kuwabadili maelfu ya wafuasi wake wa muziki kumpigia kura. Aidha, Youssou N'dour amewahi kuwashutumu viongozi wa nchi za Afrika kuhusu jinsi walivyoshughulikia janga la njaa nchini Somalia.

Historia yake

Youssou N'Dour (tamka Yusuu nduu) alizaliwa Oktoba 1, 1959, ni mwanamuziki wa Senegal na mwigizaji. Mwaka 2004, Rolling Stone alimuelezea kuwa, katika Senegal na sehemu kubwa ya Afrika, "ndiye mwimbaji maarufu kati ya walio hai." Amesaidia sana kuutangaza na kuuendeleza mtindo wa muziki maarufu nchini Senegal, unaojulikana kwa lugha ya Serer kama mbalax, aina ya muziki  ambao huelezea mbinu na mitindo yake mingi kutoka mapokeo ya kihafidhina ya muziki wa Serer wa "Njuup".

Amesaidia sana kuleta mafanikio makubwa na tuzo kwa filamu ya “Return to Goree” aliyoshiriki kuiongoza kwa kushirikiana na Pierre-Yves Borgeaud, na “I Bring What I Love” ilivyoongozwa na Elizabeth Chai Vasarhelyi, zilizotolewa na kuoneshwa katika majumba ya sinema duniani kote.

Maisha na kazi

Youssou N'Dour alizaliwa mjini Dakar kwa baba ambaye ni wa kabila la Serer. Alianza kuimba katika umri wa miaka 12. Ndani ya miaka michache alikuwa akiimba mara kwa mara na Star Band, kundi maarufu zaidi mjini Dakar katika miaka ya 1970. wanamuziki kadhaa wa Star Band walijiunga na Orchestre Baobab katika wakati huo.

Ingawa Youssou N'Dour ana uhusiano wa tamaduni za griot kwa upande wa mama yake, lakini hakulelewa katika utamaduni huo, ila alijifunza kutoka kwa ndugu zake. Wazazi wake walimtia moyo wa kutazama mambo kwa njia za kisasa zaidi, wakiacha kuzizoea tamaduni zote mbili, matokeo yake alijichukulia mwenyewe kama mtu wa kisasa katika jamii ya griot.

Mwaka 1979, alianzisha kundi lake mwenyewe, Etoile de Dakar. Kazi yake ya mwanzo na Etoile de Dakar ilikuwa katika mtindo wa kawaida wa Kilatini maarufu kote Afrika wakati huo, lakini katika miaka ya 1980 alianzisha sauti ya kipekee wakati alipoanzisha kundi lake sasa, Super Etoile de Dakar akishirikiana na Jimi Mbaye kwenye gitaa, mpiga besi Habib Faye, na Tama (mpiga ngoma) na mchezaji Assane Thiam.

Youssou N'Dour ni mmoja kati ya wanamuziki maarufu sana wa Afrika katika historia. Mwimbaji mashuhuri, mwandishi wa nyimbo, na mtunzi, mchanganyiko wa tamaduni. Ana mvuto usioegemea upande wowote kuanzia Samba ya Cuba hadi hip hop, jazz na soul zimempatia mamilioni ya mashabiki kimataifa. Katika nchi za Magharibi, Youssou ameshirikiana na wanamuziki kama Peter Gabriel, Red Axelle, Sting, Alan Stivell, Bran Van 3000, Neneh Cherry, Wyclef Jean, Paul Simon, Bruce Springsteen, Tracy Chapman, Branford Marsalis, Ryuichi Sakamoto, Dido na wengineo. Nchini Senegal, Youssou ni nyota mwenye nguvu ya utamaduni anayeshiriki kikamilifu katika masuala ya kijamii.

Amejaaliwa kuwa na vipaji mbalimbali vya ajabu, mtunzi wa nyimbo, kiongozi wa bendi, na mtayarishaji na mwenye uwezo mkubwa katika muziki. Gazeti la New York Times liliielezea sauti yake kama "Sauti nyembamba yenye kukamata, silaha nyumbufu iliyotumika kwenye mapambano na yenye mamlaka ya kinabii". Youssou N'Dour anauteka wigo wa muziki wote wa Senegal katika kazi yake.

Mwezi Julai 1993, mchezo wa kuigiza wa Kiafrika uliotungwa na Youssou N'Dour ulioneshwa katika tamasha jijini Paris nchini Ufaransa. Aliandika na kutumbuiza wimbo rasmi wa Kombe la Dunia 1998 akiwa na Axelle Red "La Cour des Grands". Youssou N'Dour aliteuliwa Balozi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) tarehe 16 Oktoba 2000.

Rasilimali kubwa ya Youssou N'Dour ni kwamba ana ufahamu mkubwa sana katika utamaduni wake. Hata kama aliamua kutafiti mahali pengine, mizizi yake ni imara. Baadhi wamekwenda mbali wakimuelezea kama Msanii wa Afrika wa Karne (jarida la Folk Roots). Ameshafanya ziara za kimataifa kwa miaka thelathini. Alishinda tuzo yake ya kwanza ya American Grammy Award (best contemporary world music album) kwa CD yake ya Egypt mwaka 2005.

Mwaka 1991 alifungua studio yake ya kurekodia, Xippi, na mwaka 1995 lebo yake mwenyewe, Jololi. Pia ni mmiliki wa L'Observateur, moja ya magazeti makubwa nchini Senegal, na kituo cha redio RFM (Radio Future Medias).

Youssou N'Doura amekuwa akijihusisha na masuala kadhaa ya kijamii na kisiasa. Mwaka 1985, aliandaa tamasha kwa ajili ya kutolewa kwa Nelson Mandela. Alishirikiswa kuimba katika matamasha ya Haki za Binadamu yalilojulikana kama Amnesty International Human Rights Now mwaka 1988, duniani kote. Ziara iliyomshirikiana Lou Reed kuchangia toleo la wimbo wa Peter Gabriel uliotolewa na Richard James Burgess na kushirikishwa kwenye albamu ya Amnesty International.

Pia amewahi kufanya kazi Umoja wa Mataifa na UNICEF na alianzisha Mradi wa Joko kwa kufungua migahawa ya intaneti katika Afrika na kuunganisha jamii ya Senegal duniani kote. Amewahi kutumbuiza katika tamasha maarufu la Live 8 (katika tamasha la Live 8, London, tamasha la Live 8, Paris na katika tamasha la Live 8, Mradi wa Edeni katika Cornwall) tarehe 2 Julai 2005, akiwa na Dido.

Mwaka 2006, Youssou N'Dour alicheza katika filamu ya kustaajabisha ya Wafrika-Waingereza (African-British abolitionist Olaudah Equiano), iliyoelezea juhudi za William Wilberforce kumaliza utumwa katika Dola ya Uingereza.

Alishiriki katika "Jealous Guy" ya John Lennon kwa CD ya 2007 Karma Instant: Kampeni ya Amnesty International Kuiokoa Darfur. Pia alishiriki katika kampeni ya pamoja ya Hispania na Senegal dhidi ya wahamiaji haramu. Youssou N'Dour alishiriki katika Soko la Hisa la mradi wa Visions mwaka 2007. Tangu mwaka 2007 amekuwa mwanachama wa baraza la World Future Council.

Mwaka 2008, Youssou N'Dour alitoa kama zawadi moja ya nyimbo zake: bebe, kwa mwimbaji wa Kifaransa, Cynthia Brown.

Mwaka 2009, aliachia wimbo wake "Wake Up (It's Africa Calling)" chini ya leseni ya Creative Commons ili kusaidia afya kimataifa katika kampeni ya IntraHealth Open ili kuleta chanzo cha maombi ya wazi ya afya kwa Afrika. Wimbo uliorudiwa ukichanganya wasanii mbalimbali ikiwa ni pamoja na Nas, Peter Buck wa R.E.M., na Duncan Sheik kusaidia kutafuta fedha kwa ajili ya kampeni.

Mwaka 2011, N'Dour ilitunukiwa shahada ya udaktari wa heshima katika Muziki kutoka Chuo Kikuu cha Yale.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa.

No comments:

Post a Comment