Oct 19, 2011

EUGENE TERREBLANCHE: Athari za uhasama wa ubaguzi wa rangi zilichangia kifo chake

Eugene Terreblanche

VENTERSDORP,
Afrika Kusini

KESI inayowahusu wafanyakazi wa shambani wawili weusi, Chris Mahlangu, mwenye umri wa miaka 29 na kijana mmoja wa miaka 16 walioshtakiwa kwa kumpiga kiongozi wa Wazungu, Eugene Terreblanche, imeanza katika mahakama moja ya Afrika Kusini tangu wiki iliyopita ambapo wanakabiliwa na kesi ya mauaji na wizi.

Watu hao wawili walijisalimisha Polisi baada ya kukiri walikorofishana na muajiri wao kutokana na malipo. Mauaji hayo yaliyotokea mwaka 2010 yalionesha wazi uhasama wa ubaguzi wa rangi ambao bado upo Afrika Kusini, miaka 16 baada ya utawala wa wazungu wachache kumalizika.

Mara tu baada ya watu hao kukamatwa kulikuwa na mzozo kati ya Waafrika na Wazungu, wafuasi wa Terreblanche katika mji wa Kaskazini-Magharibi wa Ventersdorp, ambako ndiko kesi hii inakoendeshwa na imeshaahirishwa mara mbili.

Kwa mujibu wa taarifa, waandishi habari na familia ya Terreblanche wamekaa katika chumba kimoja na kufuatilia shughuli za mahakama kwa kutumia televisheni inayopitisha shughuli hizo moja kwa moja. Vyombo vya habari vimepigwa marufuku kuingia mahakamani kutokana na kuwa mmoja wa washtakiwa hao ni mtoto.

Historia yake

Eugène Ney Terre'Blanche alizaliwa 31 Januari 1941 na kufariki mnamo 3 Aprili 2010, alikuwa mwanachama wa zamani wa Chama cha Herstigte Nasionale nchini Afrika Kusini, ambaye alianzisha Weerstandsbeweging Afrikaner (AWB) wakati wa enzi ya ubaguzi wa rangi.

Katika miaka ya 1980 na miaka ya mwanzo ya 1990, alijulikana kwa kutishia uwepo wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ili kudumisha utawala wa Wazungu wachache nchini Afrika Kusini. Baada ya nchi hiyo kuingia kwenye mpito wa demokrasia baada ya ubaguzi wa rangi, aliamsha upya misimamo yake na wito kwa wafuasi wake wa kushinikiza kuwepo kwa uhuru wa nchi huru ya Waafrikana, ambayo mara kwa mara aliitambulisha kama "Boerevolkstaat". Terre'Blanche aliongoza taasisi hiyo hadi kifo chake mwaka 2010.

Babu yake alipigana vita iliyoitwa “Waasi wa Rasi” kwa ajili ya Makaburu katika vita ya pili ya Makaburu, na baba yake alikuwa luteni kanali katika Jeshi la Afrika Kusini.

Babu yake ambaye aliitwa Terre'Blanche (jina lenye tafsiri ya 'ardhi ya weupe' au 'nchi ya weupe' kwa Kifaransa) aliyeitwa Estienne Terreblanche na alikuwa mkimbizi wa Kifaransa, kutoka jimbo la Toulon, ambaye aliwasili katika Rasi hiyo mwaka 1704, akikimbia mateso ya Waprotestanti nchini Ufaransa. Jina la Terreblanche kwa ujumla limebakia na herufi zake za awali ingawa wakati mwingine huandikwa Terre'Blanche, Terre Blanche, Terblanche au Terblans.
Alizaliwa eneo la mashambani katika mji wa Transvaal wa Ventersdorp, alihudhuria masomo katika shule za Laerskool Ventersdorp na Hoër Volkskool katika eneo la Potchefstroom, na kuingia Chuo Kikuu mwaka 1962. Wakati akiwa shule, alionesha tangu mwanzo mwelekeo wa mafunzo yake ya kisiasa kuanzisha taasisi ya kiutamaduni ya Jong Afrikanerharte (Moyo wa Waafrikana Vijana).
Alijiunga na Jeshi la Polisi la Afrika Kusini, na awali alitumikia katika eneo la Kusini Magharibi mwa Afrika (sasa Namibia), sehemu ambayo iliwekwa chini ya Afrika Kusini kwa mamlaka ya Umoja wa Mataifa baada ya Vita Kuu ya kwanza. Baada ya kurudi rasmi Afrika Kusini, alipanda na kuwa Afisa katika Kitengo Maalum, kilichoanzishwa na wajumbe wa Baraza la Mawaziri.
Kazi ya siasa

Siasa za Terre'Blanche zilitofautiana na sera za viongozi wakuu wa serikali ya weupe ya kibaguzi kwa kutaka kutambuliwa na kupewa ukuu jamii yake ya Waafrikana. Alisisitiza dhana ya Waafrikana/Makaburu kama jamii sawa ya kikabila pamoja na makabila ya asili ya Afrika Kusini. Pia alitaka uanzishwaji wa serikali ya Waafrikana ambayo itakuwa ikiongozwa na Waafrikana wenyewe katika eneo lote wanalolikalia.
Katika miaka ya 1960, Terre'Blanche alizidi kupinga kile alichokiita “sera huria” za BJ Vorster, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Afrika Kusini. Baada ya miaka minne ya huduma katika SAP, alijiuzulu ili kujiingiza katika siasa, aligombea bila mafanikio nafasi katika ofisi za mitaa katika Heidelberg kama mjumbe wa Chama cha Nasionale.

Akiwa amechoshwa na njia iliyotumika katika ushiriki wa kisiasa, Terre'Blanche alianzisha Weerstandsbeweging Afrikaner ‘AWB’ (Vuguvugu la Waafrikana) katika eneo la Heidelberg mwaka 1973, awali ilikuwa ni chama cha siri. AWB kwanza ilionekana kwa umma baada ya wanachama wake kushtakiwa na kutozwa faini. Floors van Jaarsfeld, profesa wa historia ambaye alitoa hadharani maoni yake kwamba Siku ya Nadhiri (awali ikiitwa Siku ya Dingaan), siku ya mapumziko kwa ajili ya kumbukumbu ya ‘Vita ya Mto wa Damu’, haikuwa ni kitu zaidi ya tukio la kawaida na haina kumbukumbu yoyote halisi katika historia.

Ingawa Terre'Blanche baadaye alionesha majuto yake kuhusu tukio hilo alipokuwa akitoa ushahidi wake mbele ya Tume ya Ukweli na Maridhiano, alipendekeza kwamba imani yake kuhusiana na utakatifu wa Siku ya Nadhiri itafanya matendo yake yawe ya kueleweka zaidi. Katika miaka iliyofuata, hotuba ya Terre'Blanche katika mikusanyiko ya umma mara nyingi iliamsha vita ya Mto wa Damu, na ujuzi wake ulimwezesha sana kati ya mrengo wa kulia wa weupe nchini Afrika Kusini; AWB inadaiwa kuwa na wanachama 70,000 katika urefu wake.

Katika miaka ya 1980, Terre'Blanche aliendelea kujiwasilisha mwenyewe na AWB kama mbadala kwa wote, Chama cha National kinachoongoza serikali na Chama cha Conservative, na akabaki kambi inayopinga sera ya mageuzi ya PW Botha ya kuanzisha ziada, angalau tofauti kidogo, nafasi ya ubunge kwa ajili ya wasio wazungu, na haki ya kupiga kura kwa Chotara na Waafrika Kusini wenye asili ya India. Nguvu kubwa ya wafuasi ilipatikana katika jamii za vijijini ya Kaskazini ya Afrika Kusini, pamoja na wafuasi wachache katika maeneo ya mijini ambapo kwa kiasi kikubwa alizifuatilia za jamii ya Waafrikana wa kipato cha kati na chini.

Terre'Blanche aliona kuwa mwisho wa ubaguzi wa rangi ni kama kujisalimisha kwa Ukomunisti, na kutishia kuanzisha vita kamili vya wenyewe kwa wenyewe kama Rais FW de Klerk atakabidhi madaraka kwa Nelson Mandela na African National Congress. Wakati De Klerk akishughulikia mkutano katika mji wa Terre'Blanche wa Ventersdorp mwaka 1991, Terre'Blanche aliongoza maandamano, na mapambano ya Ventersdorp yalitokea baina ya AWB na polisi, na watu kadhaa kuuawa. Terre'Blanche alidai kuwa ni wakati tu aliposimama kati ya polisi na AWB na kudai kusitishwa mapigano ndipo vurugu zilipomalizika.

Machi 2008, AWB ilitangaza kurejesha upya chama cha siasa, akitoa mfano wa faraja ya umma. Sababu za kurudi zilihusishwa hasa kutokana na mashambulizi dhidi ya wakulima na biashara za jamii ya Makaburu, matatizo ya umeme, rushwa katika idara za serikali na uhalifu mkubwa. Aprili 2008, Terre'Blanche alikuwa msemaji katika mikutano kadhaa ya kampeni ya AWB, iliyojumuisha Vryburg, Middelburg, Mpumalanga na Pretoria.

Alikuwa akitoa wito wa “Jamhuri huru ya Waafrikana”, na aliapa kupeleka kampeni yake kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Umoja wa Mataifa mjini The Hague katika jitihada za kupata alichohitaji. Alitetea ardhi kubwa iliyonunuliwa kutoka kwa kabila la Swaziland katika sehemu ya Mashariki ya Jamhuri ya Afrika ya Kusini, kutoka Kaskazini mwa Wazulu Natal, na sehemu nyingine ambayo imekuwa makazi ya Voortrekkers. Juni 2008, ilitangazwa kuwa tawi la vijana wa AWB litazinduliwa na Terre'Blanche kama mwanzilishi wake.
Septemba 2009 alihutubia mkutano wa siku 3 uliohudhuriwa na Waafrikana 300 waliokuwa na lengo la kuendeleza mkakati wa “Ukombozi wa makaburu”.

Tarehe 17 Juni 2001, Terre'Blanche alihukumiwa kifungo cha miaka sita gerezani, ambapo alitumikia miaka mitatu, kwa kumshambulia mfanyakazi wa kituo cha petroli na jaribio la mauaji ya askari wa usalama mwaka 1996. Alikanusha madai yote na alisisitiza kuwa hana hatia. Wakati alipokuwa gerezani, mmoja wa wazungu watatu waliokuwa gerezani Rooigrond karibu Mafikeng, alidai kuwa Mkristo aliyezaliwa mara ya pili.

Terre'Blanche was released on 11 June 2004 [ 46 ] and the AWB website claims these court cases and other scandals involving him were fabricated by the "Black Government and the left wing media". [ 12 ] Terre'Blanche alitolewa tarehe 11 Juni 2004 na tovuti ya AWB ilidai kuwa kesi hizi na kashfa nyingine zilizomshirikisha zilikuwa za kutungwa na “Serikali ya Weusi na vyombo vya habari vya mrengo wa kushoto.”

Tarehe 3 Aprili 2010, alipigwa na kukatwakatwa hadi kufa katika shamba lake na wafanyakazi wawili, kutokana na madai ya mshahara. Wafuasi wa Terre'Blanche wanasema kwamba mauaji hayo ni sehemu ya mkakati mkubwa wa kupambana na weupe “mauaji ya shamba” nchini Afrika Kusini.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa mashirika mbalimbali ya habari ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment