Jul 6, 2011

HUGO CHAVEZ: Kiboko ya Marekani aliyekwenda kuugulia kwa rafiki zake Cuba

Rais a Venezuela, Hugo Chavez

CARACAS
Venezuela

RAIS wa Venezuela, Hugo Chavez, wiki hii aliwahutubia maelfu ya watu mjini Caracas baada ya kutoka kupata matibabu ya saratani nchini Cuba. Wafuasi wa Rais Chavez walimshangilia kwa wingi alipowaonesha bendera ya Venezuela kutoka kwenye ghorofa ya kasri lake na kusema kuwa afya yake itaimarika.

Chavez, mwenye umri wa miaka 56, amekuwa nchini Cuba tangu Juni 8, alikofanyiwa upasuaji kuondoa uvimbe uliokuwa na vimelea vya saratani. Chavez ni rafiki mkubwa baba wa taifa wa Cuba, Fidel Castro na mtu ambaye huwa anaonekana mwiba kwa kuipasha Marekani kuacha eubabe.

Chavez, mtu mkakamavu na mwenye hotuba ndefu lakini zisizochosha alisema hatoweza kushiriki katika sherehe za kuadhimisha miaka 200 ya uhuru wa Venezuela kutoka kwa Uhispania siku ya Jumanne.

Lakini alisema kuwa atafuatilia sherehe hizo akiwa kwenye kasri ya rais. Akiwa amevaa magwanda yake ya kijeshi na kofia nyekundu, Chavez kwanza aliongoza umati huo kuimba wimbo wa taifa wa Venezuela.
"Nimerudi," alisema akiwashukuru wale wanaomuunga mkono. "Hii ndiyo dawa bora kwa ugonjwa wowote ule." Akisimama bila kusaidiwa, Chavez alizungumza kwa muda wa dakika 30 bila kuangalia popote. Maelfu ya wafuasi waliokuwa wamevaa mavazi mekundu walisema: "Hapana! Chavez haondoki!"

Awali, Chavez alisema amekuwa "na wakati mgumu" nchini Cuba lakini kwamba sasa anaendelea kupata nafuu. Chavez, ambaye ameiongoza Venezuela kwa miaka 12 na hata kunusurika jaribio la mapinduzi mwaka 2002, aliambia Televisheni ya taifa kuwa ana utaratibu kamili wa matibabu, "anatumia dawa, anatakiwa kupumzika, na kula vyakula maalum".

Mapema kulikuwa na uvumi kuhusu hali ya afya ya Chavez baada ya kuondoka Venezuela zaidi ya wiki tatu huku kila mtu akisema lake.Lakini maafisa walichosema ni kufanyiwa upasuaji.

Historia yake

Hugo Rafael Chavez Frias alizaliwa Julai 28, 1954. Alishika madaraka ya kuiongoza Venezuela mwaka 1999. Kufuatia itikadi yake ya kisiasa ya Kibolivarian na "Usoshalisti wa karne ya 21", amelenga katika kutekeleza mageuzi ya usoshalisti katika nchi kama sehemu ya mradi wa kijamii inayojulikana kama Mapinduzi ya Wabolivia, ambayo yameshuhudia utekelezaji mpya wa katiba, demokrasia shirikishi na kutaifisha viwanda kadhaa muhimu.
Alizaliwa Sabaneta, Barinas, akawa afisa kazi jeshini, na baada ya kutoridhika na mfumo wa siasa za Venezuela ambao aliuona kama wa rushwa na sio wakidemokrasia, alianzisha Vuguvugu la siri la Mapinduzi ya Kibolivarian-200 (MBR-200) katika miaka ya 1980 ili kuipindua serikali.

Baada ya tukio la kidemokrasia serikali ya Rais Carlos Perez Andres aliamuru ukandamizaji mkali wa maandamano dhidi ya kupunguzwa matumizi, Chávez aliongoza MBR-200 katika mapinduzi yaliyoshindwa dhidi ya serikali mwaka 1992, ambapo aliishia kufungwa jela.

Alipotoka gerezani baada ya miaka miwili, alianzisha chama cha siasa, Fifth Republic Movement, na alichaguliwa kuwa rais wa Venezuela mwaka 1998. Hatimaye alipendekeza katiba mpya ambayo iliongeza haki kwa makundi yaliyotengwa na ilibadilisha utaratibu wa serikali ya Venezuela, na alichaguliwa tena mwaka 2000. 
 

Wakati wa muhula wake wa pili wa urais, alianzisha mfumo wa Misheni ya Kibolivarian, Halmashauri za Kijamii na vyama vya ushirika vinavyosimamiwa na wafanyakazi, wakati pia alitaifisha viwanda mbalimbali muhimu kwa maslahi ya taifa. Wapinzani wakati huohuo, walionesha hofu kwamba alikuwa akiumomonyoa uwakilishi wa kidemokrasia na kujiongezea mamlaka, walijaribu kumwondoa madarakani kwa njia zote kupitia mapinduzi ya kijeshi yaliyoshindwa mwaka 2002 na kura ya maoni ya kukumbukwa mwaka 2003. 
 

Alichaguliwa tena mwaka 2006, kufuatia kuanzisha chama kipya cha siasa, United Socialist Party of Venezuela (PSUV), mwaka 2007.
anajulikana kama mkosoaji wa ubepari na hasa uliberali wa kisasa, Chávez amekuwa mpinzani maarufu wa sera za kigeni za Marekani. Akifungamana mwenyewe na serikali ya ujamaa ya Fidel na kisha Raul Castrol ya Cuba, ya Evo Morales wa Bolivia, na ya Rafael Correa wa Ecuador. Urais wake unaonekana kama sehemu ya “mrengo wa kushoto” ukiisafisha Amerika ya Kusini.

Amekuwa anaunga mkono ushirikiano wa Amerika Kusini na Caribbean na alikuwa mtu muhimu katika kuanzisha ushirikiano wa kanda nzima; Umoja wa Mataifa ya Amerika Kusini, Muungano wa Wabolivia kwa ajili ya Waamerika, Benki Kuu ya Kusini, na mtandao wa televisheni wa kikanda, TeleSur. Ushawishi wake wa kisiasa katika Amerika ya Kusini ulimfanya jarida la Time kumuweka katika orodha ya watu 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani katika miaka ya 2005 na 2006.

Maisha ya awali: 1954-1970

Hugo Chávez alizaliwa katika nyumba ya upande wa bibi yake mzaa baba, Rosa Inéz Chávez (aliyefariki 1982), kwenye kibanda cha matope cha vyumba-vitatu iliyoko kijiji cha Sabeneta, Jimbo la Barinas.

Wazazi wake, Hugo de los Reyes Chavez na Elena Frias de Chavez, walikuwa walimu – wa tabaka la chini kati - waliokuwa wakiishi katika kijiji kidogo cha Los Rastrojos, na kabla ya kuzaliwa Hugo walikuwa tayari na mtoto mmoja, Adan Chavez, na baada ya Hugo walipata watoto wengine watano zaidi, ingawa mmoja wao, Enzo, alikufa kwenye umri wa miezi sita. Familia ya Chávez ilikuwa ya mchanganyiko wa asili ya Amerindia, Afro-Venezuela, na Kihispania. 
 

Waliishi katika umaskini, hasa Hugo na ndugu yake Adan waliishi na bibi yao Rosa, ambaye baadae Hugo alimuelezea kuwa "binadamu safi... mwenye upendo, mwema." Alikuwa mcha Mungu, Mkatoliki, na Hugo mwenyewe alilelewa katika imani, kijana wa madhabahu ya kanisa la mtaa. Chávez alijua kwamba yeye na ndugu yake "tulikuwa maskini sana lakini watoto wenye furaha sana", na kwamba "Kwa upande wa (Rosa) bibi, nilijua unyenyekevu, umaskini, maumivu, na wakati mwingine kutokuwa na kitu chochote cha kula. Nikaona ukosefu wa haki katika dunia hii."

Mafunzo ya Kijeshi: 1971–1975

Akiwa na miaka kumi na saba, aliamua kwenda kusoma katika Chuo cha Sayansi ya Jeshi cha Venezuela mjini Caracas, baadaye alisema kwamba "nilijihisi kama samaki katika maji. Kama nimegundua sehemu ya kiini cha maisha, wito wangu wa kweli." Katika Chuo, alikuwa mwanachama wa daraja la kwanza aliyefuata mitaala ya marekebisho inayojulikana kama Mpango wa Andres Bello. Mpango huu uliwekwa na kundi la maendeleo, maafisa wa kijeshi walioamini mabadiliko yanahitajika katika jeshi.


Kazi ya awali ya kijeshi: 1976-1981

Wakati wa sherehe za kijeshi mwaka 1976. Baada ya kuhitimu, Chavez alikuwa afisa wa mawasiliano katika kitengo cha kupambana na uasi katika Jimbo la Barinas, ingawa uasi wa Marxist-Leninist ambapo jeshi lilitumwa kupambana ulikuwa umetokomezwa katika jimbo, ukitoa muda mwingi wa kitengo. Chávez mwenyewe alicheza katika timu ya baseball, aliandika makala kwenye gazeti. Katika hatua moja alikuta fasihi iliyofichwa ya ki-Marxist iliyokuwa katika gari iliyotelekezwa imejawa mashimo ya risasi. 
 

Inaonekana kilikuwa mali ya wapiganaji wa miaka mingi kabla, aliendelea kusoma vitabu hivi, ambayo ni pamoja na vile vyenye nadharia kama hiyo vya Karl Marx, Vladimir Lenin na Mao Zedong, lakini kazi aliyoipenda sana ni iliyopewa jina la Times wa Ezequiel Zamora, iliyoandikwa karne ya 19. Vitabu hivi vilimshawishi Chávez kuona haja ya mrengo wa kushoto katika serikali ya Venezuela, baadaye alisema kwamba "Kwa wakati huo nilikuwa na miaka 21 au 22, nilijiona kuwa mtu wa mrengo wa kushoto."

Kazi ya jeshi na MBR-200: 1982-1991

Miaka mitano baada ya kuianzisha ELPV, Chávez alianzisha mapambano mapya ya siri ndani ya jeshi, EBR-200, baadaye aliiboresha MBR-200. Akivutiwa na viongozi watatu wa Venezuela aliowahusudu sana, Ezequiel Zamora (1817-1860), Simon Bolivar (1783-1830) na Simon Rodriguez (1769-1854), watu hawa wa kihistoria walijulikana kama "mizizi mitatu ya mti" wa MBR-200. 
 

Baadaye alielezea msingi wa kundi hilo, Chávez alisema kuwa na "mfumo wa Bolivarian ulioanzishwa haukuwa na malengo ya kisiasa... malengo yake yalikuwa ya ndani. Juhudi zake zilielekezwa katika mahali pa kwanza pa kujifunza historia ya jeshi la Venezuela kama chanzo chetu wenyewe cha mafundisho ya kijeshi, ambacho hakikuwepo." 
 

Hata hivyo, alitumaini kwamba MBR-200 itatawala kisiasa, na mawazo yake kisiasa wakati huo, alisema kuwa "huu mti (wa Bolívar, Zamora na Rodríguez) unatakiwa kuwa mduara, unatakiwa kukubali kila aina ya mawazo, kutoka upande wa kulia, kutoka kushoto, kutoka mabaki ya kiitikadi ya wale wa zamani wa mifumo wa kibepari na kikomunusti."

Makala haya yameandaliwa na Bishop J. Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari.

1 comment: