Jun 1, 2012

KIPSANG NA KEITANY: Wakenya wanaoitangaza vyema nchi yao katika riadha

Mary Keitany

Wilson Kipsang

LONDON,
Uingereza

WILSON Kipsang na Mary Keitany kutoka Kenya walichukua ushindi kwa kishindo katika mashindano ya Jumapili ya iliyopita katika mbio za London Marathon mwaka 2012. Katika mbio za wanaume, Kipsang aliweza kuongoza katika maili saba za mwisho, na ilikuwa nusra avunje rekodi ya mashindano ya London.

Alimaliza kwa muda usiokuwa rasmi wa saa 2:04.44. Mkenya mwenzake Martin Lel alifanikiwa kumpita mwanariadha wa Ethiopia, Tsegaye Kebede, na ambaye ameshawahi kuwa mshindi wa mashindano ya London, na kumaliza katika nafasi ya pili, ikiwa ni kasi ya juu mno katika kumalizia mashindano.

Kebede, aliyemaliza wa tatu, alifanikiwa kuwazuia Wakenya kuzoa nafasi zote tatu za mwanzo kwa upande wa mbio za wanaume, lakini kwa upande wa kina dada juhudi za Waethiopia hazikufanikiwa kwani mkenya mwingine, Mary Keitany alifanikiwa kuhifadhi ubingwa wake kwa mwaka wa pili mfululizo, kwa kushinda katika muda wa 2:18.37.

Historia ya Wilson Kipsang Kiprotich

Wilson Kipsang Kiprotich amezaliwa tarehe 15 Machi 1982. Ni mkimbiaji wa mbio ndefu, anayetoa ushindani katika mbio za kuanzia km 10 hadi marathon kamili.

Anashikilia nafasi sita kwa kasi zaidi katika mbio za nusu marathon (dakika 58:59). Nafasi yake bora katika marathoni ni saa 2:03:42 aliyoiweka mwaka 2011 katika Frankfurt Marathon iliyomfanya kuwa wa pili kwa kasi katika muda wote nyuma ya Mkenya mwenziye, Patrick Makau (aliyekimbia kwa 2:03:38). Ni mshindi mara mbili wa mashindano ya Frankfurt (2010 na 2011) na pia alishinda katika mashindano ya Lake Biwa Marathon na London Marathon (2012).

Kipsang anatoka Wilaya ya Keiyo nchini Kenya, alianza ushindani wa mbio katika Polisi, na kumaliza wa pili katika kilomita 10 za Tegla Loroupe Peace. Akaanza mbio za kimataifa mwaka 2007 na mwaka huo alichukua nafasi ya pili katika mbio za Tilburg, akiweka rekodi ya muda wa 46:27, na alishinda mbio za Hem (kwa muda wa 27:51 akiwa wa nne kwa kasi katika mbio za km 10 mwaka huo). Pia alichukua nafasi ya tatu katika michuano ya Jeshi la Polisi nchini Kenya, na kumaliza nyuma ya Richard Mateelong.

Katika mashindano Bora ya Dunia ya kilomita 10, alishika nafasi ya tatu kwa muda wa 28:09, akishindwa na Deriba Merga na Sila Kipruto.

Alirudi katika mbio za Tilburg mwaka 2008, na kumaliza tena akiwa wa pili kwa sekunde mbili tu nyuma ya mshindi, Abiyote Guta. Kilele chake kwa mwaka huo kilikuwa katika Nusu Marathon za Delhi. Kipsang alimsukuma Merga, mshindi wa World Road Champion mwaka 2006, karibu kabisa na mstari wa kumalizia lakini alimaliza wa pili nyuma yake. Pamoja na kumaliza nafasi ya pili, Kipsang alifurahishwa na ubora wake kwa zaidi ya dakika 59:16. Pia alikuwa wa tatu kwa kasi katika nusu marathon kwa kwa mwaka huo, Merga na Haile Gebrselassie wakiwa mbele yake.

Kipsang alianza kwa nguvu 2009, kwa kushinda Nusu Marathon za Egmond katika hali ya baridi. Kazi nzuri nyingine ni pale alipotwaa nafasi ya pili katika mbio za Nusu Marathoni za Ras Al Khaimah - muda wake ni 58:59 uliomfanya kushika nafasi ya pili na akawa wa nne kukimbia chini ya dakika 59. Pamoja na kuwa bora mwaka 2009 katika Nusu Marathon ya Berlin, aliishia katika nafasi ya tatu ambayo ilikuwa ni mara ya kwanza, ambapo wakimbiaji wote wanne wa juu kumaliza chini ya saa moja.

Alishiriki katika mashindano ya World 10k ya Bangalore Mei 2009, na kumaliza wa nne. Alimaliza wa kwanza katika Nusu Marathoni ya Mabingwa ya IAAF mwishoni mwa mwaka huo, na kuchukua nafasi ya nne kwa muda wa 01:00:08.

Mwaka 2010 alishiriki mara ya kwanza katika mbio za Marathoni za Paris mnamo Aprili 2010, na alishika nafasi ya tatu katika muda wa saa 2:07:13, nusu dakika nyuma ya mshindi, Tadesse Tola. Alishinda katika marathoni za Frankfurt mwezi Oktoba katika rekodi mpya ya saa 02:04:57, akimshinda Tadesse kwa zaidi ya dakika. Ubora wake mpya ulimfanya kuwa wa nane kwa kasi katika muda wote. Alishinda mbio zake za tatu za Lake Biwa Marathon mwaka 2011, akimshinda Deriba Merga katika rekodi ya saa 2:06:13. Alitetea taji lake katika mbio za Frankfurt, alijitokeza ndani ya sekunde nne, kabla ya kuvuka mstari wa mwisho kwa saa 2:03:42, na kuwa mtu wa pili kwa kasi katika marathon kwa muda wote.

Mwaka 2012 alianza na kumaliza katika nafasi ya tatu katika mbio za Nusu Marathoni za RAK.

Historia ya Mary Jepkosgei Keitany

Mary Jepkosgei Keitany amezaliwa Januari 17, 1982 katika eneo la Kisok, wilaya ya Baringo. Ni mwanariadha kutoka Kenya wa mbio ndefu. Alishinda medali ya fedha mwaka 2007 katika Mbio za Dunia za Mabingwa za IAAF na akawa bingwa wa dunia katika Nusu Marathon miaka miwili baadaye. Alishinda mbio za London Marathon za 2011 kwa saa 2:19:19 zikimfanya kuwa wa nne kwa kasi kwa upande wa wanawake katika muda wote.

Rekodi yake ya muda wa saa 1:05:50 katika mbio za nusu marathoni ndiyo rekodi ya dunia kwa wanawake. Pia anashikilia rekodi ya dunia katika maili 10 kwa wanawake (dakika 50:05), kilomita 20 (62:36), na km 25 (1:19:53).

Alianza kushiriki mbio alipokuwa shule ya msingi. Mwaka 2002, alijiunga na Hidden Talent Academy. Januari 2006 alikuwa katika nafasi ya 21 katika mbio zake za kwanza (Mbio za Wanawake za Shoe4Africa, baada ya mafanikio kadhaa katika mashindano ya kitaifa, alishiriki nje ya nchi kwa mara ya kwanza, akashinda katika baadhi ya mbio za barabarani barani Ulaya).

Alishinda medali ya fedha katika Mbio za Mabingwa za Dunia za IAAF mwaka 2007, akimaliza wa pili nyuma ya Lornah Kiplagat aliyevunja rekodi ya dunia. Ameolewa na Mkenya mwenzake mwanamichezo, Charles Koech, mwishoni mwa mwaka 2007 na walipata mtoto, Jared Kipchumba 2008. Baada ya mwaka kuwa nje, alirudi katika mashindano ya Dunia ya 10k Bangalore Mei 2009. Alimaliza wa pili nyuma ya mshindi, Aselefech Mergia, lakini akaweka rekodi mpya ya ubora ya 32:09 katika km 10. Septemba mwaka huo, alimaliza kwa 1:07:00 katika mashindano ya 2009 ya Nusu Marathoni ya Lille, ambayo ilikuwa ni alama ya ushindi na akawa wa saba kwa kasi katika muda wote.

Mashindano ya Lille ilimaanisha kuwa alifuzu kwa Mashindano ya Dunia ya Mabingwa ya Nusu Marathoni ya IAAF 2009 mjini Birmingham. Alimshinda Aberu Kebede katika ushindi wake wa kwanza wa michuano ya Dunia, akaweka rekodi mpya ya ubora ya saa 1:06:36 na kuvunja rekodi ya michuano. Pia alichukua medali ya dhahabu ya pili kama sehemu ya kikosi cha ushindi cha Kenya katika mashindano ya timu. Muda wake wa km 15 wa dakika 46:51, ni bora zaidi kuliko rekodi ya dunia iliyowekwa na Kayoko Fukushi wa Japan ya 46:55. Muda wake ulikuwa wa pili kwa kasi kwa muda wote katika nusu marathon (baada ya Lornah Kiplagat) na mkurugenzi wa New York City Marathon, Maria Wittenberg, alitabiri kwamba Keitany anaweza kuwa bora ulimwenguni katika marathon katika miaka ijayo. Nusu marathon ilikuwa rekodi mpya ya Afrika, rekodi ya awali ya saa 1:06:44, iliwekwa na Elana Meyer wa Afrika Kusini mwaka 1999. Pia aliishinda rekodi ya bingwa aliyemtangulia wa Kenya ya saa 1:06:48 aliyoiweka huko Udine miaka miwili kabla.

Alishinda mbio za 2010 za Nusu Marathon za Abu Dhabi. Pia alishinda mbio za 2010 za Berlin 25K, akiweka rekodi mpya ya dunia kwa saa 01:19:53. Rekodi ya awali ilikuwa inashikiliwa na Mizuki Noguchi wa Japan tangu mwaka 2005. Alitumia mbio za Nusu Marathon za Ureno mwezi Septemba kama maandalizi kwa mbio za New York na kuongoza kuanzia mwanzo na kushinda kwa muda wa saa 1:08:46. Katika ukimbiaji wake wa kwanza katika Marathon za 2010 NYC alikuwa miongoni mwa watu watatu walioongoza lakini alishindwa katika hatua za mwisho kukamilisha katika saa 2:29:01 na kushika nafasi ya tatu.

Keitany aliuanza 2011 kwa kuvunja rekodi aliposhinda Nusu Marathon za Ras Al Khaimah na kuweka rekodi ya dunia ya 01:05:50. Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa mwanamke kukimbia kwa chini ya dakika 66 na kuweka rekodi kadhaa zingine baadaye, ikiwa ni pamoja na rekodi ya dunia ya 1:02:36 kwa km 20 na ile ya km 8 na maili 10. Kisha alishinda katika marathoni za 2011 za London katika muda wa saa 02:19:17, na kuwa wa nne kwa kasi katika muda wote kwa wanawake. Alishinda kwa mara ya pili katika mbio za Nusu Marathoni za Ureno na kuboresha rekodi yake mwenyewe kwa saa 1:07:54.

Alikusudia kuboresha rekodi yake ya dunia ya Nusu Marathoni ya 2012 RAK, lakini hali ya upepo ilimfanya kutumia muda wa saa 1:06:49 akishinda kwa muda zaidi kuliko mwaka uliopita.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari.

No comments:

Post a Comment