Jun 1, 2012

MACKY SALL: Waziri mkuu wa zamani na meneja kampeni wa rais anayeingia ikulu

Macky Sall


DAKAR,
Senegal

ALIYEKUWA rais wa Senegal, Abdoulaye Wade, amekubali kushindwa na mpinzani wake, Macky Sall, katika dura ya pili ya uchaguzi wa Urais huku hirika la habari la serikali nchini Senegal likitoa habari za kukubali kwake kushindwa.

Wade alimpigia simu mpizani wake Macky Sall, na kumuambia kuwa amekubali kushindwa. Na maelfu ya wafuasi wa Macky Sall walijitokeza katika barabara za mji wa Dakar wakisherehekea ushindi wa kiongozi wao.

Miongoni mwa waliokuwa wakisherehekea ni Bi Seynabou Seck ambaye alishindwa kuficha furaha yake kwa kusema kuwa: "Niimefurahi sana, Macky bado ni kijana na tena ni mtu mpole sana na ana heshima! Kwa hakika anastahili ushindi huu. Kila mtu alikuwa akimuombea ashinde”.

Mshindi huyo wa duru hiyo ya pili ya uchaguzi wa urais ameutaja ushindi wake kama muamko mpya kwa raia wa Senegal. Macky Sall aliyazungumza hayo mara tu baada ya mpinzani wake Abdoulaye Wade mwenye umri wa 85 kukubali kuwa ameshindwa katika duru hiyo ya pili.

Wade alikuwa anataka kuchaguliwa tena kama raia wa Senegal kwa muhula mwengine wa tatu baada ya kubadilisha katiba ya nchi hiyo. Mabadiliko hayo yalizua machafuko na vurugu kubwa nchini humo.

Machafuko hayo yalishtua ulimwengu kwani tofauti na jirani zake Senegali imekuwa tulivu na haijawahi kuwa na mapinduzi ya kijeshi kama jirani zake. Lakini upinzani ulipinga hatua ya kiongozi wao mkongwe na kwenda mahakamani. Hata hivyo, mahakama iliidhinisha hatua ya Wade ya kubadili katiba ili aweze kusimama tena kama rais.

Na baada ya duru ya kwanza kukosa kuwa na mshindi wa moja kwa moja kwani hakuna aliyepata zaidi ya asilimia 50, ikiwa ni lazima kuwe na duru ya pili ambapo viongozi wote wa upinzani walimuunga mkoni Macky Sall.

Na sasa Macky Sall ambaye zamani alikuwa Waziri mkuu katika serikali ya Abdoulaye Wade ameibuka mshindi.

Historia yake

Macky Sall amezaliwa 11 Desemba 1961. Anatarajiwa kuapishwa rasmi kuwa rais keshokutwa, Jumapili tarehe 1 Aprili 2012. Aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Senegal kuanzia Aprili 2004 hadi Juni 2007 na alikuwa Rais wa Bunge la Senegal kuanzia Juni 2007 hadi Novemba 2008. Alikuwa Meya wa Fatick kuanzia 2002 hadi 2008 na kushikilia tena nafasi hiyo tangu Aprili 2009.

Sall alikuwa mwanachama wa muda mrefu wa chama kilichotawala cha Senegal Democratic Party (PDS). Baada ya kuingia katika mgogoro na Rais Abdoulaye Wade, aliondolewa kutoka katika wadhifa wake kama Rais wa Bunge mwezi Novemba 2008, hivyo alianzisha chama chake mwenyewe na kujiunga na upinzani. Amejitokeza kuwa Rais wa Senegal tarehe 25 Machi 2012 baada ya kuishinda tawala katika uchaguzi wa marudio.

Sall, mhandisi wa jiolojia ki taaluma, alizaliwa katika eneo la Fatick. Alikuwa Katibu Mkuu wa PDS wa Mkoa wa Fatick mwaka 1998 na aliwahi kuwa Katibu wa Taifa wa PDS mkuu wa Madini na Viwanda. Alikuwa Mshauri Maalum wa Nishati na Madini kwa Rais Abdoulaye Wade kuanzia Aprili 6, 2000 hadi Mei 12, 2001, pamoja na kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya Senegal (PETROSEN) kuanzia Desemba 13, 2000 hadi Julai 5, 2001. Kisha akawa Waziri wa Madini, Nishati na Hydraulics mnamo Mei 12, 2001, na alipandishwa cheo na kuwa Waziri wa Nchi, lakini akiendelea na nafasi yake nyingine, tarehe 6 Novemba, 2002. Pia alikuwa Meya wa Fatick Juni 1, 2002.

Mnamo Agosti 27, 2003, Sall alihamishwa kutoka nafasi yake kama Waziri wa Nchi anayeshughulikia pia Madini, Nishati na Hydraulics na kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Jumuiya za Mitaa, wakati pia akiwa msemaji wa serikali. Kisha aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu na Rais Wade Aprili 21, 2004, wakati mtangulizi wake, Idrissa Seck, alipofukuzwa. Aprili 25, 2004, Seck akawa Makamu wa Rais wa PDS wa kamati ya uendeshaji.

Sall aliwahi kuwa mkurugenzi wa kampeni za Wade wakati wa uchaguzi katika uchaguzi wa rais wa Februari mwaka 2007, ambao Wade alishinda, akipata wingi wa kura katika raundi ya kwanza tu. Baada ya Wade kuapishwa, Sall aliwasilisha hati ya kujiuzulu kwake Aprili 10 na mara moja aliteuliwa tena.

Rais wa Bunge

Katika uchaguzi wa wabunge wa Juni 2007, Sall alichaguliwa kwenye Bunge kama mgombea katika orodha ya taifa ya Muungano wa Sopi. Baada ya uchaguzi, Wade alimteua kuwa Cheikh Hadjibou Soumaré kuwa Waziri Mkuu wa Juni 19, akichukua nafasi ya Sall, ambaye alikuwa amejiuzulu pamoja na serikali yake muda mfupi kabla. Sall alisema kuwa aliona fahari kwa kile alichokifanya wakati akiwa Waziri Mkuu.

Sall alichaguliwa kuwa Rais wa Bunge siku moja baadaye, mnamo Juni 20, 2007, alikuwa mgombea pekee na alipata kura 143 kutoka kwa manaibu 146 ya sasa. Sall na Wade wakaingia katika migogoro baadaye mwaka 2007 wakati Sall alipomuita mtoto wa Wade Karim, Rais wa Wakala wa Taifa wa Shirika la Kiislam (OIC), kwa ajili ya kusikilizwa katika Bunge kuhusu maeneo ya ujenzi jijini Dakar kwa Mkutano wa OIC uliopangwa kufanyika huko Machi 2008. Hii ilichukuliwa kama jaribio la Sall kutaka kudhoofisha nafasi ya Karim na uwezekano wa kushawishi ili kujijengea nafsi yake ya kuwania urais, kuchochea uadui wa Wade na wafuasi wake ndani ya PDS.

Mnamo Novemba 2007, Kamati ya Uendeshaji ya PDS iliifutwa nafasi ya Sall ya Naibu Katibu Mkuu, ambayo ilikuwa ya pili kwa madaraka katika chama, na hivyo kamati hiyo iliamua kuwasilisha muswada katika Bunge ambao uliomba kupunguza muda wa Rais wa Bunge wa kutoka miaka mitano hadi mwaka mmoja. Kufuatia kifo cha kiongozi wa kidini wa Mourides, Serigne Saliou Mbacké, mwishoni mwa Desemba 2007, mrithi wake, Serigne Mouhamadou Lamine Bara Mbacké, alimuomba Wade kumsamehe Sall; Wade baadaye alikutana na Sall na wawili walisemekana kupatana mwanzoni mwa Januari 2008.

Sall alibaki katika msuguano na uongozi wa PDS mwaka 2008.  Mwezi Septemba 2008, naibu wa PDS aliwasilisha muswada wa kupunguza muda wa Rais wa Bunge kwa mwaka mmoja, na baadaye katika mwezi huo, Sall aliitwa mbele ya Kamati ya Nidhamu ya PDS, ingawa hakujitokeza. Kwa jambo hili, Sall alishitakiwa kwa mipango binafsi ya kuleta mgawanyiko ndani ya chama, pia alidaiwa kufanya "kwa lengo la kudhoofisha chama na nchi", ikimaanishwa hasa kwa ziara ya Sall kwa Seneti ya Ufaransa na Mkataba wa 2008 wa chama cha Democratic nchini Marekani. Taarifa iliyotolewa na mshauri wa Sall wa kisiasa ililaani hatua ya kumuadabisha Sall kama "jaribio la kutaka kumfilisi kisiasa".

Oktoba 13, 2008, Bunge lilipiga kura ili kupunguza muda wa Rais wa Bunge kuwa mwaka mmoja, hii ilithibitishwa na Rais Wade Oktoba 21. Pamoja na jitihada za Sall kulinda nafasi yake, Bunge lilipiga kura ya kumfukuza katika nafasi hiyo ya Rais wa Bunge Novemba 9, 2008. Kulikuwa na kura 111 zilizotaka aondolewe na 22 dhidi ya kitendo hicho. Sall mara moja alitangaza kuwa anajiuzulu katika PDS; uamuzi huu ulimaanisha kwamba alikuwa anapoteza kiti chake katika Bunge, pamoja na kiti chake katika baraza la halmashauri ya manispaa ya Fatick na wadhifa wake kama Meya wa Fatick. Pia alisema kuwa angeunda chama kipya. Seck Mamadou alichaguliwa kuchukua nafasi ya Sall kama Rais wa Bunge la Novemba 16, 2008.

Katika upinzani

Sall ilianzisha chama chake mwenyewe, Alliance for the Republic–Yaakaar, mwanzoni mwa Desemba mwaka 2008. Wizara ya Mambo ya Ndani ilimtuhumiwa Sall kujihusisha na fedha haramu Januari 26, 2009; Sall alikanusha na kusema kuwa mashtaka yalikuwa ya kisiasa. Mwishoni mwa Februari 2009 iliamuliwa kutomshitaka Sall kutokana na kukosekana kwa ushahidi.

Kufuatia uchaguzi wa Machi 2009 wa halmashauri ya Fatick, Sall alichaguliwa tena katika nafasi yake ya mwanzo ya Meya mwezi Aprili 2009.  Alipata kura 44 kutoka kwa madiwani 45 wa manispaa wa wakati huo; madiwani watano wa Muungano wa Sopi hawakuwepo kupiga kura

Kampeni ya urais wa Senegal 2012

Matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais Februari 26, 2012 yalionesha Sall kupata asilimia 26.5 ya kura dhidi ya 34.8 za Wade, na kulazimisha kurudiwa.

Katiba na uchaguzi

Sall anapenda kurejea kwenye mipaka ya awali ya muda wa urais. Katika mzunguko wa pili wa uchaguzi wa rais, Sall alitoa wito kwa wagombea wengine wote walioshiondwa kumsaidia na kumuacha Youssou N'Dour kwa sababu aliahidi kurejesha muda wa miaka mitano kutoka muhula uliopita wa miaka saba ambao Wade alitaka urejeshwe, pia alisema atahakikisha kwamba hakuna kiongozi anaweza kubaki madarakani kwa zaidi ya vipindi viwili.

Makala haya yameandaliwa na Bishop Hiluka kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa.

No comments:

Post a Comment